Kwa lishe, mapishi na afya bora ya chakula kwa jamii

  • 1
  • 2
Prev Next

Mchanganyiko wa Maboga, Karoti, Kitunguu na Paneel Cheese

Mchanganyiko wa Maboga, Karoti, Kitunguu na Paneel Cheese

MAHITAJI 120 gram mbegu za alizeti au unaweza tumia mbegu za ufuta 1 Boga dogo, menya, toa mbegu na katakata vipande 1 kitunguu kikubwa kilichokatwa katwa 5 gram kitunguu thomu 1 karoti kubwa, kata kata vipande vya ukubwa kama kwenye picha 240 gram paneel cheese au unaweza tumia ( mushrooms/uyoga ) 1 kijiko kikubwa cha chakula korosho za kuoka zilizokatwa katwa 1 fungu la corriender na parsley kwajili ya kupambia 5 gram chuvi 5 gram pilipili manga Muda wa Kuandaa:Dakika 30   Jinsi ya kuandaa fuatilia picha na maelezo hapa chini                             Weka maboga katika...

Jinsi ya Kupunguza Uzito Wako (Diet plan) - Sehemu ya Nne

Jinsi ya Kupunguza Uzito Wako (Diet plan) - Sehemu ya Nne

  Katika sehemu hii ya mwisho, mazoezi yamepungua sana. Baada ya kukamilisha mwezi mzima wa ratiba hii na kuona mabadiliko makubwa katika mwili wako, sasa unaweza kufanya ratiba hii kuwa sehemu ya maisha yako ya kila siku. Katika mzunguko wa pili (mwezi wa pili unaofuata), unaweza kufanya mazoezi mara 3-5 kwa wiki ili kuweza kujiweka katika hali nzuri kiafya kwani ufanyaji mazoezi kupita kiasi si vizuri kwa afya yako. Pia unaweza kuanza kufanya mazoezi ya kunyanyua vitu vizito kidogo kidogo (anza...

Jinsi ya Kupunguza Uzito Wako (Diet plan) - Sehemu ya Tatu

Jinsi ya Kupunguza Uzito Wako (Diet plan) - Sehemu ya Tatu

Kuanzia siku ya 15 hadi ya 23, muda wa mazoezi umeongezeka na sit-ups pia zimeongezeka. Kama ulifuatilia kwa makini, basi nadhani umeshaanza kuona mabadiliko katika mwili wako.Wale wenye mashine ya tredmill, tembea au kimbia kwa spidi ileile kama ya siku zilizopita. Usikate tamaa, fanya ratiba hii kuwa sehemu ya maisha yako ya kila siku.   Siku ya 15 (Day 15) Asubuhi Kimbia  au tembea kwa haraka kwa muda wa saa moja (1 hour). Fanya sit-ups 50-60. Kunywa maji ya uvuguvugu (warm water) glasi 4. Mlo wa...

Jinsi ya Kupunguza Uzito Wako (Diet plan) - Sehemu ya Pili

Jinsi ya Kupunguza Uzito Wako (Diet plan) - Sehemu ya Pili

Katika muendelezo wa makala ya jinsi ya kupunguza uzito wako sehemu ya pili, leo tutaangalia namna ya kufanya mazoezi na kula kwa mpangilio kuanzia siku ya nane (8) hadi ya kumi na nne (14).   Vidokezo Muhimu Kama ulifuatilia sehemu ya kwanza, muda wa kufanya mazoezi umeongezeka ukilinganisha na zile siku saba za mwanzo, na pia siku hizi hakuna tena mazoezi ya kutembea ni kukimbia tu. Unatakiwa kukimbia polepole kwa muda wa nusu saa. Ongeza spidi kwa dakika tano, punguza dakika tano zinazofuata,...

Jenga misuli kwa kutumia iMuscle

Jenga misuli kwa kutumia iMuscle

Kama uliwahi kutembelea baadhi ya shule za bweni, haswa mabweni ya wavulana utaona ni jinsi gani vijana walivyo na ari ya kujenga maumbo yenye misuli. Kitu ambacho kitakupiga butwaa ni pale utakapoona jinsi gani wamekuwa wakifanya hivyo bila kufuata taratibu maalum. Haishangazi kuona vyuma wanavyotumia vikitofautiana uzito pia wengi wao wamekuwa na dhana moja tu, ongeza uzito na nyanyua mara nyingi. Tukirudi mtaani, ingawa wapo wenye nafasi ya kwenda sehemu za mazoezi (gyms), tatizo bado lipo palepale, wengi hatufahamu njia sahihi za kuyaendea...

Jinsi ya Kupunguza Uzito Wako (Diet plan) - Sehemu ya Kwanza

Jinsi ya Kupunguza Uzito Wako (Diet plan) - Sehemu ya Kwanza

Kuna njia nyingi sana ambazo hujaribiwa na watu ili kupunguza mwili na tumbo lakini zinakuwa ngumu sana au zinakuwa haziendani na mazingira wanayoishi hivyo kupelekea kushindwa njiani. Zipo njia za kutumia madawa kama kahawa na vinginevyo ambazo huwa si za kudumu. Kwa kuwa kahawa huwezi kutumia zaidi ya round 3 kwa maana hiyo ukinenepa tena inabidi utafute njia nyingine. Lakini njia hii ifuatayo unaweza kuifanya ikawa ni maisha yako ya kila siku ikazoeleka na ukawa unaishi hivyo hivyo bila kuongezeka...

Pancake za Unga wa Mchele na Choroko

Pancake za Unga wa Mchele na Choroko

  Leo katika makala hii, chef Issa anawaletea jinsi ya kuandaa chapati (pancake) za unga wa mchele na choroko, namna ya kupamba chakula na kukifanya kuwa cha mvuto kwa mlaji, jinsi ya kupika viazi vya kukaanga na mchanganyiko wa mboga za majani, na jinsi ya kutengeneza halwa ya karoti. Habari njema kwa wale wasiotumia nafaka aina ya ngano na wale wasiotumia mayai na wangependa sana kula chapati hizi za maji.           MAHITAJI 180 gram za mchele uliochemshwa  180 gram za mchele uwe wenye mbegu fupi nene 120 gram...

Mahanjumati ya Eid

Mahanjumati ya Eid

Leo katika mahanjumati ya Eid, tunakuletea mapishi ya biriani ya nyama ya ngombe, biriani na sosi ya nyama ya mbuzi, mandi na nyama, makbuus dajaaj, maandazi, mchuzi wa kima na mayai, nyama ya kukaanga na pilipili manga, juisi ya tikiti maji na embe, juisi ya mabungo na juisi ya mapera na karakara. Wapikie familia yako vyakula vitamu wafurahie sikukuu vizuri.   1. Biriani Nyama ya Ngombe    Vipimo Vya Masala    Nyama vipande                          ...

Mapishi

Mapishi (7)

Saturday, 20 August 2011 06:44

Mapishi ya Futari 2

Written by
Katika muendelezo wa makala ya mapishi ya futari sehemu ya pili, leo tunakuletea mapishi ya chapati, mbaazi kwa mchicha, mbaazi za nazi, uji wa kunde na juisi ya kuondoa sumu mwilini.

 1. Chapati za Ngano
 












Vipimo

4 Vikombe vya unga wa ngano mweupe 
3 Vijiko vya kulia vya samli safi 
2 Vijiko vya chai vya chumvi 
2 Vikombe vya maji vuguvugu
Samli ya kupika chapati 

Namna ya Kutayarisha na Kupika
  1. Mimina unga, samli na chumvi kwenye sinia au bakuli kubwa. Changanya pamoja.
  2. Mimina maji kidogo kidogo huku unachanganya na ule mchanganyiko wa unga.
  3. Mchanganyiko ukishashikana, kanda unga kwa mkono kiasi, kama dakika tano
  4. Funika na uache mchanganyiko kwenye sinia kama dakika kumi hivi kwa   kuufunika ili hewa isiingie.
  5. Maandalizi ya ChapatiGawanya ule mchanganyiko kwa kufanya madonge kama kumi na nne au kumi na sita kwa chapati ndogo.
  6. Mimina unga kidogo mahali ambapo utasukuma chapati.
  7. Sukuma donge moja mpaka liwe duwara jembamba.
  8. Paka samli kama kijiko kimoja cha kulia, ukihakikisha umepaka duwara lote.
  9. 9. Kunja lile duwara kama mfano wa kamba, huku unazungusha kama kamba ili iwe ndefu kidogo.
  10. Zungusha ile kamba iwe mviringo. Funika na kitambaa kisafi cha jikoni ambacho kimajimaji kidogo.
  11. Endelea namna hii mpaka umalize madonge yote.
  12. Sukuma chapati iwe mviringo kama nchi 7 hivi 
  13. Pika chapati kwenye frying pan moto wa kiasi. Ikiiva upande mmoja na kuanza kufura/kuvimba, geuza upande wa pili. Tumia kitambaa kisafi cha jikoni kugandamizia na kuzungusha zungusha ile chapati. Ikiiva upande wa pili, mimina kijiko kimoja cha kulia cha samli na ugeuze chapati tena, zungusha zungusha kisha mimina nusu kijiko cha kulia cha samli na ugeuze upande wa pili kidogo. Toa chapati uweke kwenye sahani. Ikunje kunje kidogo kisha uifungue vizuri.
  14. Endelea namna hii huku unafuta frying pan na kitambaa  kisafi au karatasi za jikoni (tissue) baada ya  kila chapati.
Kidokezo
 
Maandalizi ya Chapati













Unapomaliza kuzipika kila moja, zitandaze kwanza chapati katika sahani (au sinia) kubwa zipate kupoa ziwe kavu ili zisinyonye mafuta. Kisha tena ziweke katika sahani yako ya kawaida. 

 











Ni nzuri kutolea na jam au asali

Chapati kwa Jam au Asali













Unaweza ku freeze chapati katika Freezer bags. Kunja chapati  moja moja ziwe nusu. Zifunike na Wax paper, kisha zitie kwenye freezer bags na uzihifadhi katika freezer. Unapotaka kula, toa kwenye freezer na upashe moto katika Microwave. Unaweza kula kwa mbaazi za mchicha, mbaazi za nazi, maharage ya nazi au ya samli/mafuta, choroko za nazi, kunde za nazi, au mboga yoyote ile upendayo.

 Namna ya Kuhifadhi Chapati











2. Mbaazi za Mchicha kwa Chapati

Mbaazi kwa Mchicha












Vipimo

Mchicha uliokatwa katwa (chopped)                        400 gm au vikombe 3  
Mbaazi mbichi au kavu                                            1 kikopo au vikombe 2
Kitunguu                                                                  Kimoja
Nyanya kopo                                                           ½ kijiko cha chai
Tui la nazi zito                                                         1 kikombe
Chumvi                                                                    Kiasi
Pilipili mbichi nzima                                                    2

Namna ya Kutayarisha na Kupika
  1. Ikiwa mbaazi sio za tayari, loweka uchemshe hadi ziive.
  2. Osha vizuri mchicha kisha, katakata  mdogo mdogo (chopped) au tumia ulio tayari wa barafu (frozen chopped spinach) 
  3. Katika sufuria, tia mchicha pamoja na mbaazi zilizokwisha iva.  
  4. Katakata kitunguu, utie humo, tia nyanya kopo, tia chumvi na pilipili mbichi nzima .
  5. Tia tui upike katika moto mdogo mdogo hadi zitokote na kuiva mchicha, usiache zikauke sana. Tayari kuliwa na chapati, maandazi au wali.
3. Mbaazi za Nazi

Mbaazi za Nazi













Vipimo
 
Mbaazi za kopo                                    2 au nusu kilo
Kitunguu                                              1
Chumvi                                                Kiasi
Manjano (curry powder )                      ½ Kijiko cha chai
Kidonge cha supu (curry cube)            Kipande kidogo
Mafuta                                                1 Kijiko cha chai
Pilipili mbichi                                       2 Nzima
Nazi                                                    3 ½ Vikombe

Namna ya Kutayarisha  na Kupika
  1. Osha mbaazi kwenye chungio na ziache zitoke maji.
  2. Kaanga kitunguu kidogo tu kisha tia mbaazi na majano.
  3. Tia kidonge cha supu na chumvi pilipili mbichi na nazi
  4. vikombe vitatu, utabakisha nusu kikombe.
  5. Ikisha kauka kidogo changanya nazi ya unga kama
  6. Vijiko 4 vya supu kwenye nazi uliobakisha, mimina kwenye mbaazi
  7. Iache motoni kidogo hadi iwe nzito na itakuwa tayari kuliwa kwa maandazi au chapati.
4. Uji wa Kunde

  Uji wa Kunde











Vipimo

Kunde Kavu                                                  2 Vikombe
Tui                                                                1 Kikombe 
Sukari                                                           1 Kikombe
Maji                                                              7 Vikombe  
Garam masala                                              ½ Kijiko cha chai
Hiliki                                                              Kiasi
Karafuu                                                         3-4 Chembe
Pilipili manga                                                 ½ Kijiko cha chai
Chumvi                                                          Kiasi

Namna ya Kutayarisha na Kupika  
  1. Chemsha kunde kavu bila ya kuloweka kwa maji vikombe 4 na sukari kikombe kimoja kwa moto kiasi mpaka ziive
  2. Kisha mimina vitu vyote vilivyobakia pamoja na  maji vikombe 3 vilivyobaki na acha ichemke taratibu mpaka maji yapunguke uji uwe mzito.
  3. Epua mimina kwenye bakuli  na tayari kwa kuliwa.
5. Juisi ya Kuondoa Sumu Mwilini (Detoxifying Juice)

Juisi ya kuondoa Sumu Mwilini












Vipimo

Majani ya Kale (kale leaves)                                   3
Brokoli pamoja na miche yake                                ½ msongo
Kabeji iliyokatwa pamoja na zizi lake                      ½
Nyasi majani (fennel)                                             1
Tufaha (apples)                                                      2

Mboga ya Majani ya KaleNamna ya kutayarisha
  1. Katakata vitu vyote vipande weka katika bakuli
  2. Tia katika mashine ya kukamua juisi, washa mashine ikamue juisi.
  3. Mimina katika gilasi ikiwa tayari kunyiwa   
Kidokezo
 
Juisi hii ni ya kuondosha athari za sumu (toxins) zinazokusanyika mwilini na kusababisha maradhi mbali mali. Kutumia kwake kila baada ya muda kunasaidia kusafisha damu na kumuhifadhi mtu na athari za sumu.

Nyasi Majani (fennel leaves)





















Shukrani kwa tovuti ya www.alhidaaya.com kwa makala hii.



Monday, 08 August 2011 03:57

Mapishi ya Futari

Written by
Ni kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani. Ni kipindi cha mfungo kwa ndugu Waislam kote duniani. Kwa kulitambua hilo, wavuti yako ya http://www.tanzmed.com itakuwa ikikuletea makala mbalimbali kuhusu mapishi ya aina mbalimbali ya futari za mwezi huu wa Ramadhani. Vyakula hivi pia vinaweza kupikwa hata na wale ambao hawako kwenye mfungo wa mwezi wa Ramadhani, kwa wakristo wakati wa kwaresma au siku yoyote ile.
  1. Pilau ya  Sosi ya Soya na Mboga









Vipimo
 
Kuku (mkate vipande vipande)                                                1
Mchele wa Basmati (lowanisha)                                               3 magi (1 mug)
Mdalasini                                                                                1 mche mmoja                      
Vitunguu maji (vilivyokatwa vyembamba)                                6
Mchanganyiko wa mboga za barafu                                         1 magi (1 mug)
(karoti, mahindi, njegere)
Kabichi (iliyokatwa katwa nyembamba)                                   1 magi (1 mug)
Pilipili mbichi (iliyosagwa)                                                        3
Pilipili boga iliyokatwa vipande vidogo vidogo                           1
Pilipili manga                                                                           1 kijiko cha chakula
Chumvi                                                                                   1 kijiko cha chakula
Sosi ya soya (soy sauce)                                                         5 vijiko vya chakula
Kotmiri iliyokatwa katwa                                                          1  magi (1 mug)
Thomu na tangawizi iliyosagwa                                                2 vijiko vya chakula

Namna ya Kutayarisha na Kupika 
  1. Tia mafuta ndani ya karai. Yakipata moto kiasi, mimina vitunguu maji na mdalasini 1 mzima kaanga. Itachukua muda kidogo. Kaanga mpaka viive viwe rangi ya hudhurungi (brown). Viepue na uweke kando.
  2. Ndani ya sufuria kubwa, mimina kuku, chumvi, thomu (kitunguu thomu) na tangawizi, sosi ya soya, pilipili manga, pilipili mbichi, chemsha mpaka kuku aive na maji yakauke.
  3. Changanya vitunguu  ulivyokaanga, kabichi, pilipili, mboga, kotmiri, mchanganyiko wa mboga za barafu na weka kwa muda wa dakika tano au kumi. Tia na mafuta kidogo uliyokaangia vitunguu .
  4. Chemsha mchele na chumvi uive kama kawaida ya kupika wali wa kuchuja (wali wa maji). Ukishauchuja umwagie katika masala ya kuku.
  5. Nyunyizia mafuta kidogo uliokaangia vitunguu.
  6. Weka moto mdogo mpaka wali ukishaiva, uchanganye ukiwa tayari kwa kuliwa.
Dokezo

Unaweza kuupika wali huo ndani ya jiko, yaani badala ya kutia masala kwenye sufuria ukayatia katika bakuli au treya (tray) ya jiko (oven), kisha ukamwagia wali uliouchuja humo na kuupika katika moto wa nyuzi joto 400-450  kwa muda wa dakika 15-20.

2. Kabaabu za Kuchoma katika Vijiti













Vipimo
 
Nyama ya kusaga                                   3 lb (au kilo moja na nusu)
Thomu                                                   1 kijiko cha chakula        
Tangawizi                                               1 kijiko cha chakula
Chumvi                                                   Kiasi
Kotmiri                                                   1 msongo
Bizari ya kababu                                      ½ pakiti ya 100g
(Shan Chapplin Kabaab mix)
                                              
Namna ya Kutayarisha na Kupika  
  1. Saga nyama pamoja na kotmiri mara mbili iwe laini kuliko ya  sambusa.
  2. Tia kwenye bakuli na changanya na vitu vyote pamoja.
  3. Viringisha kwenye vijiti vya kuchomea na acha kama muda wa saa.
  4. Choma (bake) katika oven kwa moto wa 350?c  mpaka zigeuke rangi na kuiva.
  5. Zikishaiva ziweke kwenye sahani tayari kwa kuliwa na saladi, chips, mikate au wali.   
Dokezo
  1. Ni vema kuloweka vijiti vya kuchomea kwenye maji usiku nzima ili ukichoma  kababu vijiti visiungue.
  2. Tumia bizari zako mwenyewe upendazo ikiwa huna hiyo ya Shan Chapplin Kabaab Mix.
3. Sharbati ya Maziwa na Shira ya Rozi













Vipimo
 
Shirah ya Rozi (rose syrup)                             ½ kikombe cha chai
Vipande vya barafu                                          1 Kikombe cha chai
Maziwa                                                            4 Kikombe cha chai 

Namna ya Kutayarisha
  1. Tia maziwa, shirah ya rozi na barafu katika jagi la kusagia (blender)
  2. Saga kwa muda wa dakika moja au mbili.
  3. Mimina sharbati kwenye gilasi ikiwa tayari.
Shukrani za Kipekee kwa tovuti ya http://www.alhidaaya.com kwa kututumia makala hii.

Kwa niaba ya timu nzima ya Tanzmed tunawatakia mfungo mwema wa mwezi wa Ramadhani. Ramadhan kareem..
Saturday, 02 July 2011 06:28

Jinsi ya Kuandaa Chakula cha Mtoto

Written by

Mtoto ale chakula muda gani?

Chai ya asubuhi: Saa 12:00 mpaka 2:00 kutegemeana na ni muda gani mtoto anakwenda shule. Jambo la muhimu ni kuwa, mzazi/mlezi ahakikishe mtoto anakula asubuhi ili asiende shle akiwa na njaa, ikibidi mzazi/mlezi amfungie mtoto chakula abebe.

Chakula cha mchana: Muda wa kati ya saa 5:30 mpaka saa 7:00 mchana.

Chakula cha jioni: Saa 10:00

Chakula cha usiku: Saa 1:00 usiku

Jinsi ya kuandaa chakula cha siku ya Jumatatu

Asubuhi: Kifungua kinywa (Breakfast)

Mlo 1: Chapati Maji Na Juisi Ya Chungwa

Mahitaji: 250 gram Unga wa ngano, 1 yai, 100 gram maziwa ya maji, 20 gram mafuta ya mahindi, 10 gram baking powder

Jinsi ya kuandaa chapati maji: Changanya vitu vyote katika bakuli kisha piga na mchapo mpaka upate mchanganyiko safi na laini kabisa. Iwapo mchanganyiko bado mzito ongeza maji kiasi.

Jinsi ya kuandaa juisi ya chungwa: Menya chungwa safi kabisa ili kuondoa uchungu wa gesi iliyopo katika maganda. Kisha tumia chombo maalumu cha kukamulia juice, kamua kisha hifadhi katika friji bila kuweka sukari ili ikae kwa muda bila kuharibika. Kumbuka pia kuweka sukari wakati wa kunywa.

Mlo 2: Uji wa Ulezi na Mtindi

Mahitaji: 200 gram unga wa ulezi, 100 gram maziwa ya maji, 350 gram maji, 100 gram mtindi usio na ladha ya matunda

Jinsi ya kuandaa uji wa ulzei na mtindi: Changanya unga wa ulezi na maziwa katika bakuli kisha chukua sufuria weka maji kiasi cha gram 350. Chemsha maji yakishachemka weka mchanganyiko wa maziwa na unga wa ulezi koroga mpaka uchemke na kuchanganyika safi kabisa ili uji wako usishike chini na kuungua. Acha uchemke vizuri kisha onja ukipata ladha ya kuiva kwa nafaka utakua tayari.

Toa jikoni weka katika bakuli litakalotumiwa na mtoto kisha changanya mtindi usio na ladha ya matunda pamoja na sukari tayari kwa mtoto kunywa.

Mchana: Chakula cha mchana

Mlo: Glass ya maziwa na mkate wa nyama za kusindika

Jinsi ya kuandaa: Mpatie mtoto 200 gram za maziwa sawa na glasi moja ya uvuguvugu au ya baridi lakini kumbuka yawe yamechemshwa vizuri na yakapoa kwa ajili ya usalama.

Kisha chukua vipande viwili vya mkate paka siagi au mayonaisi. Kisha chukua beef salami na beef backon weka kati kati pamoja na slice ya nyanya na tango mbichi mpatie mtoto ale.

Jioni: Chakula cha jioni

Mlo: Sahani ya mchanganyiko wa mboga mbichi

Jinsi ya kuandaa: Chukua caroti, tango, pilipili hoho nyekundu na ya kijani zote mbichi na zuchini ichemshe kidogo kisha weka mtindi wenye ladha ya matunda kwa ajili ya kulia hizo mboga.

Huu ndio muonekano wa sahani ya mchanganyiko wa mboga kama mtoto ni mdogo sana zisage kwenye mashine ya kusagia nyama kisha utapata mchanganyiko laini mpatie mtoto asiyeweza kutafuna hizo mboga mbichi.

Usiku: Chakula cha usiku

Mlo 1: Supu ya uyoga

Mahitaji: 300gram Uyoga fresh au wa kopo, 50 gram kitunguu maji, 10 gram kitunguu swaumu, 10 gram tangawizi, 50 gram leeks, 100 gram viazi mbatata, 100 gram maziwa fresh, 50 gram mafuta ya kupikia, 300 gram maji

Jinsi ya kuandaa supu ya uyoga: Kaanga katika mafuta ya kupikia vitunguu maji na vitunguu swaumu pamoja na tangawizi. Kisha weka viazi mbatata, leeks na uyoga kaanga tena kiasi kisha weka maziwa na maji acha ichemke mpaka viazi viive kisha toa na saga kwenye blenda. Rudisha jikoni kama itakuwa nzito sana ongeza maziwa au maji kiasi. Usisahau kuweka chumvi kulingana na ladha.

Mlo 2: Kuku maziwa, muhogo na njegere

Mahitaji: 200 gram nyama ya kuku isiyo na mifupa, 100 gram njegere, 200 gram maziwa, 150 mihogo iliyochemshwa kwanza, 300 gram maji

Kulia ni machine ya kusagia nyama utakayoitumia kwa ajili ya kusagia vyakula mbali mbali.

Jinsi ya kuandaa kuku maziwa, muhogo na njegere: Chemsha vyote kwa pamoja kuku na njegere mbichi pamoja na muhogo uliokwisha chemshwa kwanza mpaka ikaribie kukauka mchuzi  kisha toa jikoni. Chuja kisha weka mchuzi pembeni.

Chukua mchanganyiko wa njegere, kuku na muhogo. Tumia machine ya kusagia nyama weka huo mchanganyiko kisha saga upate rojo zito kisha rudisha katika sufuri, changanya na ule mchuzi uliochuja ongeza chumvi kulingana na ladha mpe mtoto ale chakula kikiwa cha moto.

Kama huna mashine ya kusagia nyama tumia mwiko kuponda itakua safi kabisa kisha unachanganya na ule mchuzi uliochuja.

Kwa mtoto mkubwa usisage. Baada ya kuchemsha ikaiva ongeza chumvi kisha mpakulie ale chakula cha moto atafurahia sana mchanganyiko wa ladha ya chakula hiki.

Orodha kwa ajili ya manunuzi siku ya Jumatatu

Uyoga wa kopo au fresh, mihogo mibichi, pili pili hoho, tangawizi, unga wa ngano, mayai, maziwa, sukari, chumvi, njegere, nyama ya kuku, tango, zucchini, mtindi usio na ladha ya matunda, mtindi wa ladha ya matunda, baking powder, viazi mbatata, mafuta ya mahindi na leeks.

Vitu hivi vyote sio vingi na unaweza kuvitumia siku inayofuata maana menu yetu ina uwiano safi kabisa. Vitu vingi vinatumika karibu kila siku na manunuzi yake sio ghali kabisa. Mpe mwanao raha kwa kula chakula safi na salama.

Kwa maelezo zaidi, tembelea blog ya www.activechef.blogspot.com ambapo Chef Issa anachambua na kuelezea namna ya kuandaa mapishi mbali mbali kwa ufundi na ubora wa hali ya juu. Kwa mawasiliano, unaweza kumuandikia kupitia email yake ya This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Fuatilia Makala

Maoni Mapya